Loading...

Programu ya Kiutalaamu (Takhassus)

Programu ya kielimu yenye isnadi kwa mujibu wa mbinu ya kielimu iliyodhibitiwa, inajumuisha idadi ya viwango na hatua za masomo, inalenga kutoa mwanafunzi aliyebobea katika elimu za Sharia na Fani zake, na hii ni maalumu kwa mwenye juhudi na uwezo wa kujitolea katika nyakati zilizopangwa, kwa sababu masomo yamewekewa muda maalumu kulingana na ratiba ya masomo kwa kila somo (Kozi), na masomo yake yanajumuisha mikutano ya moja kwa moja na walimu na nafasi ya majadiliano, na shughuli na baadhi ya kazi za nyumbani na utaratibu makini katika mitihani, na ni lazima kwa mwanafunzi kufuatilia masomo na kuwasilisha kazi zinazotakiwa kulingana na ratiba iliyoandaliwa.

Video ya utangulizi wa programu

Jinsi ya kusoma

Ngazi za programu ni tatu. ngazi ya kwanza husomeshwa kwa lugha ya kiswahili kisha ngazi nyengine kwa lugha kiarabu . Mwanafunzi akitaka shahada ya kuhitimu kutoka katika akademia, anatakiwa kukamilisha ngazi zote. Anaweza pia kusoma ngazi moja au masomo maalumu; akimaliza hupata cheti cha kukamilisha ngazi au kozi.

Usajili wa kozi hufunguliwa kwa muda wa majuma mawili. Unafungwa moja kwa moja idadi ya nafasi zikikamilika. Kozi huanza baada ya usajili kumalizika iwe idadi imekamilika au la

Kila kozi mpya huanza katikati ya kozi inayoendelea. Faida zake:

Kuongeza idadi ya wanaokubaliwa — nafasi inapatikana mwaka mzima.

Uratibu mzuri wa makundi: wanafunzi wapya huongezeka kwa utaratibu bila msongamano

Masomo hufanyika siku tano kwa wiki: Jumamosi hadi Jumatano.
Alhamisi na Ijumaa ni mapumziko.
Kila siku hufunguliwa somo moja

Vikao vya Moja kwa Moja

Kwa lengo la kuongeza ufahamu, maswali na majadiliano:

Kozi zenye chini ya masomo 25: kikao kimoja katikati ya kozi

Kozi zenye masomo 25 au zaidi: vikao viwili (katikati ya kozi, na kabla ya masomo mawili ya mwisho)

Mwanafunzi anatakiwa kuhudhuria kikao cha moja kwa moja; akikosa kwa sababu ya udhuru rasmi, hurekodiwa na kufidiwa.


Mtihani wa somo: maswali ya kuchagua (MCQ) baada ya kila somo. Kiwango cha ufaulu 80%.

Majukumu: tafiti na kazi za kimasomo katika baadhi ya kozi. Hawezi kufungua somo lijalo bila kukamilisha mahitaji ya somo lililotangulia.

Mtihani wa mwisho: Mwanafunzi huchagua tarehe ndani ya majuma mawili baada ya kozi kuisha. Kiwango cha ufaulu 70%. Akifeli, anaruhusiwa mtihani wa marudio baada ya wiki moja

 

Ukifaulu kozi: cheti cha kukamilisha kozi.

Ukikamilisha ngazi nzima: cheti cha kukamilisha ngazi.

Ukikamilisha ngazi zote tatu: shahada ya kuhitimu kutoka akademia