Loading...

Programu Maalumu (Takhassus)

Programu ya kielimu yenye isnadi (iliotegemezwa) kwa mujibu wa mbinu ya kielimu iliyodhibitiwa, inajumuisha idadi ya viwango na hatua za masomo, inalenga kutoa mwanafunzi aliyebobea katika elimu ya Sharia na Fani zake, na hii ni maalumu kwa mwenye juhudi na uwezo wa kujitolea katika nyakati zilizopangwa, kwa sababu masomo yamewekewa muda maalumu kulingana na ratiba ya masomo kwa kila somo (Kozi), na inajumuisha katika kusoma hapo mikutano ya moja kwa moja na walimu na nafasi ya majadiliano, na shughuli na baadhi ya kazi na utaratibu sahihi katika mitihani, na ni lazima kwa mwanafunzi kufuatilia masomo na kuwasilisha kazi zinazotakiwa kulingana na ratiba iliyoandaliwa.

Video ya utangulizi wa programu

Jinsi ya kusoma

Ngazi za programu: Ngazi za program ni tatu (ngazi ya kwanza husomeshwa kwa Kiswahili na ngazi mbili kwa kiarabu) Mwanafunzi akitaka shahada ya kumaliza Chuo lazima apite ngazi zote na amalize kwa ufaulu, anapaswa mwanafunzi kusoma ngazi inayotakiwa na mtaala uliowekwa, akimaliza kwa ufaulu anapewa shahada ya kumaliza ngazi au ya kukamilisha mtaala

Muda wa usajili: Unafunguliwa usajili kwa ajili ya kozi (Somo) kwa muda wa wiki mbili na unafungwa usajili moja kwa moja baada ya kukamilika idadi iliopangwa na masomo huanza baada ya muda wa usajili kumalizika sawa sawa idadi imekamilika au haijakamilika

Mfumo wa usajili wenye kuendelea: Kila kozi mpya huanza katikati ya kozi iliotangulia, Faida za mfumo huu: 

1. Kuongeza idadi ya wanaokubaliwa: inaachiwa idadi kubwa ya wanafunzi iwezekanavyo kujiunga na masomo mwaka wote

2. kupangilia vizuri Mikupuo: Wanafunzi wapya wanajiunga kwa mpangilio wa kawaida bila msongamano 

Siku za Masomo: Siku tano kwa wiki kuanzia Jumamosi hadi Jumatano. (Alkhamis na Ijumaa ni mapumziko) kwa kila siku hufunguliwa kipindi kimoja katika Somo

Vikao vya moja kwa moja: Na hilo ni kwa ajili ya kuhakikisha uwezo na ufahamu mzuri wa Mtaala na kuongeza ukaribu katika mchakato wa usomeshaji, na muda wa mkutano ni saa moja kama ifuatavya:-

1.    Somo lenye vipindi chini ya 25, kunakua na mkutano mmoja tu katikati ya Kozi

2.    Somo lenye vipindi 25 na zaidi, kunakua na mikutano miwili, Katikati ya kozi na kabla ya vupindi viwili vya mwisho katika mtaala (Ni lazima kwa mwanafunzi kukushiriki mkutano wa moja kwa moja kwa sababu mkutano huo ni katika yanayotakiwa kwenye somo na anapata maksi, na mwenye dharura inayojulikana na inayokubaliwa atapewa badala yake nafasi ya kufuatilia audio)


Mtihani wa somo: Maswali kwa njia ya kuchagua (Chagua jibu sahihi) baada ya kila somo na wastani wa ufaulu ni 80%.

Kazi: Kazi na majukumu ya kufanya Tafiti katika baadhi ya masomo na mitaala (Mwanafunzi hafunguliwi somo la pili isipokua baada ya kukamilisha mtihani na yanayotakiwa katika soma la kwanza

Mtihani wa mwisho: Anaweza mwanafunzi kuchagua tarehe ya mtihani ndani ya wiki mbili baada ya kozi kuisha na anachagua siku na muda kwa mujibu wa nafasi yake. Wastani wa ufaulu hapo ni (70%) Mwanafunzi akifeli hapo, anaweza kufanya mtihani wa marudio baada ya wiki moja tangu kufanyika mtihani wa kwanza

Pindi Mwanafunzi akifaulu katika kozi anapewa cheti cha kumaliza mtaala, na akimaliza masomo yote ya ngazi kwa ufaulu anapewa cheti cha kumaliza ngazi, na akimaliza ngazi zote kwa ufaulu anapewa Shahada ya kumaliza Chuo.